Baraka FM

Jamii yatakiwa kutumia mazao ya nyuki kuijiimarisha kiuchumi

17 February 2026, 15:46

Hawa ni waratibu wa kongamano la ufugaji nyuki mkoani Mbeya(Hobokela Lwinga)

Zao la nyuki linatajwa kuwa na faida mbalimbali za kiafya na kiuchumi.

Na Hobokela Lwinga

Vijana wametakiwa kuchangamkia fursa za ufugaji wa nyuki kwa ajili ya kujiongezea kipato hali itakayopunguza malalamiko ya ukosefu wa ajira nchini.

Rai hiyo imetolewa na mkurugenzi wa kampuni ya GeoAfrrica consultant Lukelo Mgana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea kwenye kongamano la vijana linahusu uzalishaji wa mazao ya nyuki linalotarajiwa kufanyika mwezi machi,mwaka huu.

Sambamba na hayo amesema Zaidi ya vijana 500 watashiriki katika kongamano hilo,mgeni rasmi anatarjiwa kuwa ni waziri wa nchi ofisi ya rais ,maendeleo ya vijana Joel Nanauka na mgeni mwalikwa akiwa ni Waziri mkuu mstaafu Mizengo Peter Pinda.

Mkurugenzi wa kampuni ya GeoAfrrica consultant Lukelo Mgana(Picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mkurugenzi wa kampuni ya GeoAfrrica consultant Lukelo Mgana

David Lyama ambaye ni mfugaji nyuki kibiashara mkoani Mbeya na mwakilishi wa kampuni ya ufugaji nyuki TABEDO,amesema sekta ya ufugaji nyuki imeweza kutoa ajira zaidi ya milioni mbili, huku akishauri mamlaka zinazohusika na ufugaji kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na ufugaji bora wa nyuki.

David Lyama ambaye ni mfugaji nyuki kibiashara mkoani Mbeya na mwakilishi wa kampuni ya ufugaji nyuki TABEDO(Picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya David Lyama ambaye ni mfugaji nyuki kibiashara mkoani Mbeya na mwakilishi wa kampuni ya ufugaji nyuki TABEDO