Baraka FM

Mwenyekiti Mch Simkwembe ahidi ujenzi Ofisi mpya

15 February 2026, 18:03

Mch Simkwembe mwenyekiti KMT-JKM wilaya ya Mbeya(picha na Hobokela Lwinga)

Wachungaji na waumini watakiwa kushirikiana katika ujenzi wa miundombinu ya kanisa kwa hali na mali

Na Hobokela Lwinga

Mwenyekiti wa kanisa la Moravian wilaya ya Mbeya mchungaji Greenwell Sinkwembe amewataka wakristo katika wilaya yake kujitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu Ikiwa ni sambamba na ujenzi wa ofisi za wilaya na nyumba za watumishi.

Baadhi ya waumini walio hudhuria Ibada hiyo(picha na Hobokela Lwinga)

Kauli hiyo ameizungumza katika ibada ya kumpokea kuanza rasmi kuanza kazi katika wilaya Mbeya,iliyofanyika katika kanisa la Moravian ushirika wa mabatini jijini Mbeya.

Aidha mch.Sinkwembe amewaomba wakristo kuwa chanzo cha Amani na kuepuka migogoro ndani na nje ya kanisa hali itakayosaidia maendeleo mbalimbali ya kanisa na taifa.

Baadhi ya waumini(picha na Hobokela Lwinga)

Kwa upande wake mwenyekiti wa wilaya ya uyole mchungaji Godfrey Tinga wakati akihubiri amesema kanisa linapaswa kuhubiri Amani,kwani Amani ni msingi wa mambo mengi.

mchungaji Godfrey Tinga(picha na Hobokela Lwinga)

Akizungumza kwa niaba ya wachungaji wenzake mchungaji Jonam Msangawale amesema wako tayari kuumuunga mwenyekiti wako katika kutekeleza majukumu yake ya ujenzi wa kanisa.