Baraka FM

Wahitimu vyuo watakiwa kutumia ujuzi wao kwa uaminifu ili kuweza kuaminika na wateja wao

26 November 2025, 14:00

Wanafunzi wahitimu katika picha ya pamoja na mgeni rasmi na viongozi wengine wa chuo,serikali na waalikwa(picha na Hobokela lwinga)

‎Ufundi stadi una umuhimu mkubwa katika kusaidia kunguza changamoto ya ajira kwa watu wengi.‎‎

Na Hobokela Lwinga

‎‎Wahitimu wa vyuo vya ufundi nchini wametakiwa kutumia fani zao walizosomea kwa kujiajiri ili kujiinua kiuchumi  na kuachana na malalamiko ya ukosefu wa ajira.

Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi Mchungaji Nsevilwe Msyaliha akimkabidhi cheti kwa mmoja wa wanafunzi wahitimu(picha na Hobokela Lwinga)

Rai hiyo imetolewa na Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi Mchungaji Nsevilwe Msyaliha akiwa mgeni Rasmi Katika mahafali ya tisa ya chuo cha ufundi Ilindi kinachomilikiwa na Jimbo hilo kilichopo wilaya Mbeya mkoani Mbeya.

‎‎Aidha Katibu Mkuu huyo amewataka wahitimu katika chuo hicho kuwa waaminifu katika shughuli zao hali itakayo wapa kuaminiwa na wateja wao.‎‎

Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi Mchungaji Nsevilwe Msyaliha(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi Mchungaji Nsevilwe Msyaliha

Akizungumza kwa niaba Mkurugenzi wa mipango na uchumi  na maendeleo kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi Esau Swillah,Afisa kilimo wa jimbo hilo Benjamin Masasi amewataka wahitimu kuzingatia ujuzi walioupata.

Afisa kilimo wa Kanisa la Moravian Tanzania jimbo la kusini magharibi Benjamin Masasi(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Afisa kilimo wa Kanisa la Moravian Tanzania jimbo la kusini magharibi Benjamin Masasi

‎‎Hata hivyo mkuu wa chuo cha Ufundi Moravian Ilindi Paul Fataki amesema utoaji wa elimu inayotolewa chuoni hapo imekuwa ikizingatia utoaji wa elimu inayoweza kumsaidia mhitimu kujiajiri pasipo kutegemea kuajiriwa.‎‎

Mkuu wa chuo cha Ufundi Moravian Ilindi Paul Fataki(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mkuu wa chuo cha Ufundi Moravian Ilindi Paul Fataki

Akisoma risala kwa niaba ya wanafunzi wenzake wahitimu Agatha Anyandwile amesema chao kimekuwa msaada makubwa wa kupunguza changamoto za ajira kwa vijana wengi.‎‎

Mwanafuzi mhitimu Agatha Anyandwile
Sauti ya Mwanafuzi mhitimu Agatha Anyandwile