Baraka FM

Askofu Pangani afungua mkutano mkuu “sinodi”KMT-JKM,awataka wajumbe kuepuka kampeni za kupata viongozi

21 October 2025, 22:55

‎‎Askofu wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Robert Pangani(picha na Hobokela Lwinga)

Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi kila baada ya miaka mitano linafanya mkutano mkuu.

‎‎Na Hobokela Lwinga

‎‎Askofu wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Robert Pangani amewataka wajumbe wa mkutano mkuu wa kanisa hilo” Sinodi”kujiepusha na kampeni za kupata viongozi badala yake wajikite kumuomba Mungu ili kupata viongozi waliokusudiwa na Mungu mwenyewe.‎‎

Baadhi ya wajumbe wa kamati tendaji (kulia)ni makamu mwenyekiti KMT-JKM mchungaji Asulumenie Dickson Eva Mwahalende na kushoto)ni Katibu Mkuu KMT -JKM mchungaji Nsevilwe Msyaliha

Rai hiyo ameitoa wakati akifungua mkutano mkuu huo wa sinodi unaofanyika katika ukumbi wa wilaya ya Mbeya kanisa, uliopo nanenane jijini Mbeya.‎‎

Hawa ni baadhi ya wajumbe wa halmashauri kuu ya kanisa, KMT-JKM.

Aidha Askofu Pangani ameyataja baadhi ya mafanikio ambayo kanisa limeyapata kwa miaka mitano iliyopita kuwa kufanikiwa kufungua kituo cha runinga cha Baraka Tv.‎‎

Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wamesema matarajio yao ni kupata viongozi wenye hofu ya Mungu na kuhakikisha kanisa linasonga mbele kiroho na kimwili.

Baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa 14 wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa wilaya ya Mbeya KMT -JKM

Mkutano huo wa sinodi huwa unafanyika kila baada ya miaka mitano lengo likiwa ni kufanya tathimini ya maendeleo mbalimbali ya kanisa sambamba na kupata viongozi wapya wanaochaguliwa na wajumbe wa mkutano.