Baraka FM

Dkt.Mpango mgeni Rasmi kilele mbio za mwenge

14 October 2025, 08:04

Dkt Mpango akiwa Kwenye ibada maalumu ya kumuombea hayati Mwl Nyerere(picha na Ezra Mwilwa)

kuelekea kilele cha mbio za mwenge wa Uhuru na kumbukizi ya kifo cha baba wa Taifa Mwl Julius Nyerere mwakamu wa rais mgeni rasmi mkoani Mbeya.

Na Ezra Mwilwa

Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango, ashiriki Ibada katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Fransisco wa Asili, Mwanjelwa mkoani Mbeya.

lbada maalumu ya kumuombea Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Viongozi wa Imani wakiongoza ibada maalumu kumuombea hayati Mwl Nyerere (picha na Ezra Mwilwa)

Pamoja na kushiriki lbada hiyo, leo Oktoba 14, 2025, Makamu wa Rais atakuwa mgeni rasmi kwenye kuhitimisha Wiki ya Vijana Kitaifa ambayo maonesho yake yalikuwa yakifanyika katika Viwanja vya Uhindini, Mbeya.

Waziri akishiriki Ibada kumuombea hayati Mwl Nyerere (picha na Ezra Mwilwa)

Baadae atashiriki kwenye sherehe za kilele cha mbio za Mwenge na kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa katika Viwanja vya Sokoine, Mbeya.