Baraka FM

Chagua njia nyembamba si ndefu-Askofu Pangani

11 September 2025, 18:02

Askofu Robert Pangani KMT-JKM(picha na Ezra Mwilwa)

Wanadamu wametakiwa kujachungu njia nyembamba itakayo wasaidia kuurithi ufalme wa mbinguni siku ya mwisho.

Na Ezra Mwilwa

Askofu wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Mch. Robert Pangani amewataka wakristo na watu wote kuchagua njia njema inayompendeza mungu ili waweze kurithi ufalme wa mbinguni.

Rai  hiyo katika Ibada ya mazishi ya MCH Ambakisye Ngonya iliyofanyika katika kanisa la Moravian Ushirika wa ZZK uliopo mji mdogo wa mbalizi mkoani Mbeya.

Baadhi ya wachungaji wakiwa wamebeba mwili wa marehe Mch Ngonya(picha na Ezra Mwilwa)
Sauti ya Askofu Mch Robert Pangani

Mch Laurence Nzowa mwenyekiti wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Mbozi na Mch Luka Kamwela katibu wa wilaya ya Mbalali Wamesema enzi za uhai wa Mch Ngonya amelitumikia kanisa kwa kuanzisha miradi mbalimbali.

Mch Laurence Nzowa( picha na Ezra Mwilwa)
Sauti za Mch Laurence Nzowa na Mch Luka Kamwela

Raphael Mlwafi kwa niaba ya familia na ukoo wa Ngonya amewashukuru viongozi wa kanisa na watu wote walio shiriki katika safari ya kumsindikiza mpendwa wao.

Baadhi ya washiriki katika msiba huo(picha na Ezra Mwilwa)
Sauti ya Raphael Mlwafi