Baraka FM

Vijana watakiwa kufanya maamuzi sahihi ili kuyafikia malengo ya maendeleo yao ya badae

25 June 2025, 12:08

Picha ya pamoja kati ya viongozi wa udiakonia, wakufunzi wa semina na washiriki (picha na Hobokela Lwinga)

Elimu haina mwisho kauli hiyo inathibitisha kuwa elimu haichagui umri wa mtu,bali elimu ni msingi wa maendeleo kwa mtu na taifa.‎‎

Na Hobokela Lwinga

‎‎Kaimu Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Nsevilwe Msyaliha Ameitaka Jamii hasa vijana kuwa na maamuzi sahihi  ambayo yatakuwa na mstakabali wa maisha yao ya maendeleo ya sasa na ya badae huku wakimtegemea Mungu.‎‎

Mch.Msyaliha ameyasema hayo wakati akifungua semina ya wazazi na walezi wa watoto yenye lengo la kutoa Elimu ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi iliyofanyika katika kituo cha kulea watoto yatima kilichopo ndani ya chuo cha Moravian  Chunya mkoani Mbeya kinachomilikiwa na kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi, Semina iliyoandaliwa na idara ya udiakonia na kufadhiliwa na shirika la mission 21.‎‎

Sauti ya ‎‎Kaimu Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Nsevilwe Msyaliha

Katika hatua nyingine Mch.Msyaliha amewataka washiriki Katika Semina hiyo kuzingatia yale yanayofundishwa na wakufunzi kwani yanafaida zaidi kwenye malezi.‎‎

‎‎Kaimu Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Nsevilwe Msyaliha(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya ‎‎Kaimu Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Nsevilwe Msyaliha

Akifundisha ugonjwa wa UKIMWI katika Semina hiyo afisa mradi kutoka udiakonia Emmanuel Angetile amesema tafiti zinaonyesha kuwa maambukizi ya ukimwi nchini kwa watu ni elfu sitini kwa kila mwaka.‎‎

Afisa mradi kutoka udiakonia Emmanuel Angetile (Picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya afisa mradi kutoka udiakonia Emmanuel Angetile

Kwa upande wake mkufunzi wa udiakonia katika semina hiyo Lulu Mpenja amesema kuna umuhimu mkubwa wa kuwasaidia watu wenye uhitaji kwani kufanya hivyo ni kumwakilisha Mungu katika utendaji wake duniani.‎‎

Mkufunzi wa udiakonia akizungumza umuhimu wa kusaidia wahitaji Lulu Mpenja(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mkufunzi wa udiakonia katika semina ya udiakonia Chunya Lulu Mpenja

Baadhi ya washiriki katika Semina hiyo wamelishukru Kanisa huku wakisema elimu waliyoipata itawasaidia wao na watu wanaowazunguka.

Washiriki wakiwa kwenye Semina (picha na Hobokela Lwinga)
Sauti za baadhi ya washiriki katika Semina

‎‎Aidha katika semina hii watoto na wazazi wamepewa zawadi mbalimbali ikiwemo sukari, mafuta ya kupakaa,vifaaa vya shule Pamoja na bima za afya ambavyo vimetolewa na msimamizi wa vituo vya kulea yatima vya kanisa la Moravian Mch.Elizabeth Nampasa.‎‎

Baadhi ya watoto wakipokea zawadi(picha na Hobokela Lwinga)

Huu ni mwendelezo wa seminar za udiakonia zinazoendelea kutolewa kwa watumishi wa kanisa la Moravian pamoja na vyuo vyake ,idara zake ikiwemo za kulea watoto yatima.‎