Baraka FM

FUWAVITA yaitunuku cheti Baraka fm kwa kutoa na kuanda maudhui ya kupigania haki za watu wenye ulemavu

16 June 2025, 19:00

Mfanyakazi wa redio Baraka fm Hobokela Lwinga akipokea cheti kutoka kwa mgeni rasmi Raphael Shitindi

Thamani ya mtu iko mikononi vivyo hivyo thamani ya taasisi iko mikononi mwa mtu pia.

Na Hobokela Lwinga

‎Katika kuthamini mchango wa uandaaji wa maudhui ya kupigania haki za watu wenye ulemavu Shirika la Tanzania Joy Women Entrepreneurship for the Deaf (FUWAVITA) lenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam limekitunuku kituo cha redio Baraka fm radio kinachomilikiwa na kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi.

‎Cheti hicho kimetolewa wakati wa kufunga mafunzo ya ujasiriamali kwa watu wenye ulemavu yaliyofanyika katika ukumbi wa kanisa la Moravian ushirika wa Rujewa wilayani Mbarali mkoani Mbeya.

‎Katika wa cheti hicho  yameongozwa na Baba askofu Robert Pangani wa KMT -JKM akiongozana na mwandishi na Mtangazaji wa Redio Baraka @Hobokelalwinga.