Baraka FM

Viongozi wa dini himizeni wakristo kuombea uchaguzi

19 May 2025, 17:53

Askofu Robert Pangani wa kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi(picha Deus Mellah)

Viongozi wa dini nchini wametakiwa kuwahimiza wakristo kuendelea kuombea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu ili uweze kufanyika kwa amani na wapatikane viongozi wenye maono.

Kufuatia tukio kubwa la uchaguzi wa viongozi mbalimbali ndani ya taifa letu mwaka huu 2025 Askofu Robert Pangani amewahimiza viongozi wa dini kuwahamasisha wakristo kuomba juu ya tukio hilo,na viongozi wa kanisa kwa ujumla

Na Deus Mellah

Wito huo umetolewa na Askofu wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini Magharibi Mch Robert Pangani wakati akizungumza na waumini katika ibada ya maombi ya kuliombea taifa na kanisa hilo.

Sauti ya Askofu wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini Magharibi Mch Robert Pangani

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu wa Kanisa la Moraviani Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Mchungaji Sevilwe Msyaliha amesema kazi ya kanisa ni kuombea viongozi wake na taifa kwa ujumla.

Kaimu Katibu Mkuu wa Kanisa la Moraviani Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Mchungaji Sevilwe Msyaliha(kushoto wa kwanza)
Sauti ya Kaimu Katibu Mkuu wa Kanisa la Moraviani Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Mchungaji Sevilwe Msyaliha

Naye katibu idara ya uwakili jimbo Mchungaji Paul Mwambalaswa amesema maombi hayo yatakuwa yanafanyika mara kwa mara katika sehemu mbalimbali ndani ya kanisa la Moraviani Jimbo la Kusini Magharibi.

Sauti ya katibu idara ya uwakili jimbo Mchungaji Paul Mwambalaswa

Baadhi ya waumini kutoka madhehebu mbalimbali wameshiriki katika maombi hayo na kuupongeza uongozi wa kanisa la moravian jimbo la kusini magharibi chini ya Askofu Robart Pangani

Baadhi ya wakristo walio shiriki maombi hayo(picha na Deus Mellah)
Sauti za waumini kutoka madhehebu mbalimbali wameshiriki katika maombi hayo