Baraka FM

TAKUKURU Mbeya yaokoa upotevu wa fedha milioni 15 za mikopo ya 10%

8 May 2025, 19:10

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa mbeya Maghela Ndimbo(picha na Hobokela Lwinga)

Jukumu la kuzuia vitendo vya rushwa katika jamii ni suala la kila mtu kwani rushwa imekuwa ni adui wa haki na kusababisha kukwama kwa maendeleo.

Na Hobokela Lwinga

Taasisi ya  kuzuia na kupambana na rushwa mkoa wa Mbeya TAKUKURU imefanikiwa kuokoa shilingi milioni 15 kutoka katika  kikundi cha YOUTH REVOLUTION GROUP zilizotokana na mikopo ya asilimia kumi ya halmashauri iliyotolewa katika halmashauri ya wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.

Taarifa hiyo imetolewa na mkuu wa TAKUKURU mkoa wa mbeya Maghela Ndimbo wakati akizungumza na wandishi wa habari katika ukumbi wa ofisi yake kuhusu mafanikio ya utendaji kazi kwa miezi mitatu january – machi 2025.

Baadhi ya wanahabari wakitekeleza majukumu yao katika ukumbi wa ofisi za TAKUKURU mkoa wa Mbeya
Sauti ya mkuu wa TAKUKURU mkoa wa mbeya Maghela Ndimbo

Aidha Ndimbo amesema wamefanikiwa kurejesha eneo la ekari nne kwa mamlaka ya mji mdogo wa Mbalizi zilizouzwa kinyume na taratibu,sheria na miongozo ya uendeshaji wa mamlaka.

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa mbeya Maghela Ndimbo(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mkuu wa TAKUKURU mkoa wa mbeya Maghela Ndimbo

Katika hatua nyingine mkuu huyo Amewataka wananchi kutoa taarifa za rushwa kuelekea kipindi cha uchaguzi october,2025 pindi wanapoona kwenye maeneo yao huku akisema taasisi yake inaendelea kutoa elimu juu ya athari za  rushwa.

Sauti ya mkuu wa TAKUKURU mkoa wa mbeya Maghela Ndimbo