Baraka FM

KKKT waanda kambi ya madaktari bingwa wa macho,Mbeya

23 April 2025, 18:24

Askofu Geoffrey Mwakihaba wa kanisa la KKKT Dayosis ya Konde(picha na Ezra Mwilwa)

Kutokana na changamoto ya watu wengi kukumbwa na tatizo la macho,KKKT Dayosisi ya Konde wameandaa kambi ya madaktari bingwa watakao toa matibabu kwa wiki moja bure mkoani Mbeya.

Na Ezra Mwilwa

Askofu Geofrey Mwakihaba wa kanisa la KKKT dayosisi ya konde amewataka wakristo na watu wote wanyanda za juu kusini kushiriki katika uzinduzi wa hospital mpya ya kibigwa itakayo ambatana na marathon yenye lengo la kusaidia watu wenye matatizo ya macho mkoani Mbeya.

Askofu Mwakihaba amesema hayo katika uzinduzi wa marathoni hiyo ambapo ameeleza kuwa fedha zitakazopatikana zitaelekezwa katika ununuzi wa vifaa tiba na kugharamia matibabu kwa watu wenye changamoto ya macho itayotolewa na madaktari bingwa kutoka hospital ya KCMC.

Askofu Mwakihaba katika Ibada ya uzinduzi wa Marathoni (picha na Ezra Mwilwa)
Sauti ya Askofu Mwakihaba akieleza kuhusu kambi ya madaktari Bingwa

Aidha askofu Mwakihaba amesema  katika kuelekea uchaguzi mkuu mwaka huu kila anayetamani kutia nia asitumie rushwa.

Sauti ya Askofu Mwakihaba akieleza kuhusu Uchaguzi

Mkurugenzi wa Idara ya Afya na udiakonia Daktari Lee Mmwakalinga amesoma risala mbele ya Askofu akieleza maomba mbalimbli kutoka Idara hiyo.

Mkurugenzi wa Idara ya Afya Daktari Lee Mwakalinga(picha na Ezra Mwilwa)
Sauti ya Daktari Lee Mwakalinga

Mwenyekiti wa kamati ya marathon Angumbwikye Mwalupogo amesema katika kipindi cha kambi ya madaktari bingwa Kila mwenye changamoto ya macho ajitokeze kupata matibabu hayo.

Mwenyekiti wa kamati ya Marathon Angumbwikye Mwalupogo(picha na Ezra Mwilwa)
Sauti ya Angumbwikye Mwalupogo

Nao baadhi ya wakisto wamesema watu wa Mbeya watumie fursa hii kupata tiba.

Baadhi ya waumini walio hudhuria Ibada hiyo(picha na Ezra Mwilwa)
Sauti za baadhi ya waumini