Baraka FM

Moravian yakusanya milioni 30 harambee ununuzi wa gari

26 March 2025, 17:32

Askofu wa kanisa la Moravian KMT-JKM Mch Robert Pangani

Katika kuhakikisha urahisi wa utendaji kazi shughuli za kikanisa, kanisa la Moravian wilaya ya Mbalizi wamefanya harambee ya ununuzi wa Gari

Na Hobokela Lwinga

Viongozi wa Kanisa la Moraviani Tanzania wilaya ya Mbalizi wametakiwa kuendelea kufanya kazi kwa ueledi na ufanisi ili kuhakikisha kanisa linapiga hatua kubwa kimaendeleo.

Askofu Mch. Robert Pangani(Picha na Hobokela Lwinga)

Hayo yamesemwa na Askofu wa kanisa hilo Mch. Robert Pangani wakati wa ibada ya harambee kwa ajili ya ununuzi wa gari iliyofanyika kanisa la Moraviani ushirika wa Yeriko na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali.

Askofu Pangani amesema fedha zote zilizokusanywa kupitia harambee hiyo zielekezwe kwenye lengo lililokusudiwa na kwamba hivi sasa kanisa linataka kuongeza magari kwa ajili ya ofisi ya katibu mkuu.

Kwaya ya Kesheni wakiwa na katika picha ya pamoja na viongozi wa wilaya ya Mbalizi na mgeni rasmi bw.Yona Sonelo(wa tatu kulia) waliokaa.

Hata hivyo Mwenyekiti wa wilaya ya mbalizi kanisa la Moravian mchungaji Erica Samwanijembe amewashukuru watu wote waliofanikisha zoezi la uchangiaji.

Mwenyekiti wa wilaya ya mbalizi kanisa la Moravian mchungaji Erica Samwanijembe akitoa maelezo kwa mgeni rasmi bw.Yona Sonelo (kulia)kuhusu ujenzi wa ofisi za wilaya yake(kushoto)

Zaidi ya shilingi milioni thelathini zimepatikana katika harambee ya ununuzi wa gari ya kanisa la Moravian wilaya ya Mbalizi.