Baraka FM

Mke wa marehemu mchungaji Kalengo afariki dunia, kanisa la Moravian laomboleza

15 March 2025, 18:18

Utaratibu na ratiba ya maziko ya marehemu Kalengo Salome Magwaza

Kifo kifo hakichagui mtu, safari hiyo kila mtu ni lazima aipitie kwa wakati wake na kwa njia yake.

Na Hobokela Lwinga, Mbeya

Aliyekuwa mke wa mchungaji marehemu Kalengo Salome Magwaza amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa Kanda ya Mbeya.

Akitoa taarifa ya msiba huo, Makamu mwenyekiti na Kaimu Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Asulemenye mwahalende amesema marehemu amefariki machi 14,2025.

Makamu mwenyekiti na Kaimu Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Asulemenye mwahalende

Aidha katika taarifa ya mchungaji Mwahalende amesema marehemu Salome Magwaza ataagwa jumapiili machi 16,2025 majira ya saa kumi kamili alasiri katika ushirika wa Nzovwe Moravian na atazikwa jumatatu machi 17,2025 katika kijiji cha Matula-Mbozi mkoani Songwe.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa kifo cha mama mchungaji Salome Magwaza kimetokana na ajali aliyoipata wiki mbili nyuma.

Marehemu Kalengo Salome Magwaza