Baraka FM

Kabudi ataka vyombo vya habari kuzingatia ufasaha wa lugha ya kiswahili

13 February 2025, 13:42

Mwanekano wa juu ukionyesha washiriki wa mkutano wa wadau wa vyombo vya Habari nchini (picha na Charles Amlike)

Kulingana na mchango wa vyombo vya habari katika maendeleo ya nchi,TCRA imewakutanisha wadau kujadili na kujifunza mambo mbalimbali kuelekea uchaguzi Mkuu 2025.

Na Charles Amlike,Dodoma

Waziri wa habari,utamaduni,Sanaa na michezo Prof.Paramagamba Kabudi amevitaka vyombo vya habari viache kubananga lugha ya kiswahili badala yake vitumie misamiati sahihi ya lugha hiyo.

Waziri kabudi ameyasema hayo wakati akifungua mkutano Mkuu wa vyombo vya habari leo tarehe 13 Februari, 2025 dunia ikiwa inaadhimisha siku ya vyombo vya habari duniani katika ukumbi wa new generation jijini Dodoma unapofanyika Mkutano Mkuu wa wadau wa vyombo vya habari uliandaliwa na mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA.

Waziri wa habari,utamaduni,Sanaa na michezo Prof.Paramagamba Kabudi(picha na Charles Amlike)

Aidha Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA Dkt. Jabiri Kuwe Bakari amevitaka vyombo vya habari kuwa na utaratibu wa utunzaji wa Takwimu.

Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA Dkt. Jabiri Kuwe Bakari (picha na Charles Amlike)

Katika hatua nyingine Msemaji Mkuu wa serikali na katibu Mkuu wizara ya habari, utamaduni sanaa na michezo Gerson Msigwa, ameishukuru na kuipongeza TCRA kwa kuwa na Jukwaa la kuwakutanisha wadau wa sekta ya habari pamoja.

Msemaji Mkuu wa serikali na katibu Mkuu wizara ya habari, utamaduni sanaa na michezo Gerson Msigwa(picha na Charles Amlike)

Mkutano huo unakwenda na kauli mbiu isemayo wajibu wa vyombo vya habari kuelekea uchaguzi Mkuu 2025

Baadhi ya washiriki wa mkutano