Baraka FM

TAKUKURU Mbeya yarejesha zaidi milioni 15 kwa wasafirisha sampuli za binadamu

29 January 2025, 16:34

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Maghela Ndimbo(picha na Hobokela Lwinga)

Jukumu la kupambana na kuzuia Rushwa si la taasisi ya TAKUKURU pekee bali kila mwananchi anao wajibu wa kutoa taarifa za Rushwa pindi anapobaini mianya katika eneo alilopo.

Na Hobokela Lwinga, Mbeya

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa mkoa wa Mbeya imefanikiwa kurejesha fedha zaidi ya milioni 15 kwa wananchi kutoka taasisi ya kimarekani inayoitwa Henry Jackson foundation medical research international HJFRMI yenye makao makuu yake mkoani Mbeya.

Akitoa taarifa ya utendaji kazi ya miezi mitatu kuanzia October hadi disemba 2024,Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Maghela Ndimbo amesema taasisi yake imeshinda kesi hiyo dhidi ya bw.Emmanuel Malewo ambaye alijipatia kama rushwa kwa wasafirisha sampuli za binadamu katika wilaya ya Mbarali.

Huu ni mwonekano wa nje jengo la TAKUKURU Mbeya(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Maghela Ndimbo

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya amesema wamebaini uwepo wa mianya ya upotevu wa mapato yatokanayo na ukataji wa leseni za biashara katika halmashauri ya jiji la Mbeya.

Sauti ya Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Maghela Ndimbo

Aidha amesema TAKUKURU mkoa wa Mbeya umefanikiwa kuwafikia wananchi 54,224 kwa kuwapatia elimu ya kuzuia vitendo vya Rushwa.

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Maghela Ndimbo(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Maghela Ndimbo

Sanjari na hayo Ndimbo amesema kwa miezi mitatu ijayo January hadi machi itaendelea na ya TAKUKURU Rafiki kwa kufanya mikutano ya hadhara kila mwezi kwa ngazi ya kata kwa lengo la kuibua kero mbalimbali.

Sauti ya Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Maghela Ndimbo

Mkuu huyo wa TAKUKURU ametumia fursa hiyo kuwaasa wananchi kufuatilia na kuhoji hatua za utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyopo kwenye maeneo yao ili kudhibiti ubadhirifu wa fedha za miradi hiyo.

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Maghela Ndimbo(picha na Hobokela Lwinga)