Baraka FM

Vijana wa kanisa la Moravian washiriki mkutano na kujifunza neno la Mungu

14 October 2024, 13:41

Hawa ni baadhi ya vijana walikuwa katika ibada ya hitimisho la mkutano (picha na Hobokela Lwinga)

Takribani siku nne vijana wa kanisa la Moravian wamekuwa na Mkutano wa kujifunza neno la Mungu.

Na Hobokela Lwinga

Vijana kati kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi wamehitimisha Mkutano wao mkuu wa Jimbo uliofanyika katika ushirika wa Mkwajuni mkoani Songwe.

Akizungumza na vijana hao wakati Wa kuwasilisha salamu za Jimbo, Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi ndugu Israel Mwakilasa amesema lengo Mikutano hiyo ni kujiungamanisha na Mungu sambamba na kumshukru Mungu katika matendo makuu anayoyafanya kwa kila mtu na kanisa.

Sauti ya Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi ndugu Israel Mwakilasa

Sambamba na hayo Mwakilasa amewataka vijana hao kutunza amani ya kanisa na taifa kwa ujumla.

Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi ndugu Israel Mwakilasa(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Katibu Mkuu kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi ndugu Israel Mwakilasa

Akihubiri katika ibada ya kufunga mkutano huo katibu Wa wilaya ya Mbeya mch.Nuru Mwamahonje amesema vijana wanapaswa kumtumikia Mungu kwa kuachana na uovu unaotendeka duniani.

Katibu Wa wilaya ya Mbeya mch.Nuru Mwamahonje(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya katibu Wa wilaya ya Mbeya mch.Nuru Mwamahonje

Aidha katibu wa idara kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Abel Mbise amewataka vijana kuepuka mafundisho ya uongo yanayotolewa na baadhi ya watu wanaojiita watumishi Wa Mungu.

Sauti ya katibu wa idara kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Abel Mbise

baadhi ya washiriki wa mkutano huo wamesema Mkutano huo umekuwa na faida kwani wamejifunza mambo mbalimbali huku wakilishukru kanisa kwa kuwezesha Mkutano huo.

Sehemu ya kwaya ya dinari ya Iwindi Mbalizi wakiimba katika mkutano huo(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti za baadhi ya washiriki wa Mkutano

Katika mkutano huo vijana hao wameweza kuonyesha vipawa mbalimbali ikiwemo usomaji Wa Biblia, kujifunza masomo ya uchumi, utandawazi ndoa pamoja na uimbaji.