Baraka FM

UWSA Mbeya kuongeza mtandao wa maji taka

19 July 2024, 17:29

afisa uhusiano wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mkoa wa mbeya Neema Stanton(picha na Sifael Kyonjola)

Na Sifael Kyonjola

Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mkoa wa Mbeya imepanga kuongeza mtandao wa maji taka  na kukarabati ili kuwafikia  wateja wengi zaidi.

Hayo yamesemwa na kaimu meneja wa mamlaka ya maji safi  na usafi wa mazingira mkoa wa Mbeya mwandishi Samwel Mmakasa wakati akizungumza na kituo hiki juu ya uboreshaji wa miundo mbinu ya maji taka.

Mmakasa amesema mamlaka hiyo itaendelea kuboresha mifumo ya maji taka ambayo imeenea kwa asilimia 14 na una urefu wa kilomita 138 kjwa wakazi wa jiji la Mbeya.

Kaimu meneja wa mamlaka ya maji safi  na usafi wa mazingira mkoa wa Mbeya mwandishi Samwel Mmakasa(picha na Sifael Kyonjola)

Kwa upande wake afisa uhusiano wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mkoa wa mbeya Neema Stanton amesema wanakabiliana na changamoto ya wizi wa mifuniko ya chemba pamoja na utupaji wa taka ngumu katika chemba hizo.

Afisa uhusiano wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mkoa wa mbeya Neema Stanton

Mmoja wa madiwani wa jiji la Mbeya Henry Mwangambaku amesema wananchi wanatakiwa kuitumia vizuri mifumo ya maji taka ambayo imepunguza gharama za uchimbaji wa mashimo ya vyoo.

Henry Mwangambaku diwani kata ya forest jijini Mbeya (picha na Sifael Kyonjola)