Baraka FM

Mch Mstaafu Mwaisango waumini ombea Tanzania

5 October 2025, 11:45

Mch Nelson Mwaisango(picha na Ezekiel Kamanga)

kuelekea uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29,Oktoba 2025 viongozi wa dini wameendelea kuhimiza waumini kuombea taifa ili kuvuka salama.

Na Ezekiel Kamanga

Mchungaji Nelson Mwaisango Mwenyekiti pia Katibu mstaafu wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini amewataka waumini wa Kanisa la Moravian Tanzania kuombea amani nchini hasa kipindi hiki cha uchaguzi ili waendelee kulitangaza neno la Mungu bila vikwazo.

Baadhi ya waumini walio shiriki Ibada hiyo(picha na Ezekiel Kamanga)

Mchungaji Mwaisango ameyasema hayo katika ibada iliyofanyika Ushirika wa Nyibuko lililopo Kijiji cha Syukula Kata ya Kimo Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya.

Amesema nchi nyingine hushindwa kumuabudu Mungu kutokana na vita vilivyopo katika nchi zao hivyo kila muumini atenge muda wa kuiombea amani nchi yetu na Kanisa kwa ujumla.

Mch Mwaisango (picha na Ezekiel Kamanga)