Baraka FM

Baraka FM, wadau wake wawapa tabasamu wafungwa Ileje Songwe

1 September 2025, 19:39

Baadhi wa wadau wakikabidhiana zawadi mbalimbali kwa baadhi ya viongozi wa gereza(picha na Hobokela Lwinga)

Vitabu vya dini vinatuasa kuishi maisha ya kusaidia wengine kwani hakuna ambaye aliumbwa kwa mategemeo ya kukumbana na changamoto duniani.

Na Hobokela Lwinga

Kituo cha Redio Baraka kinachomilikiwa na kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi kimewashukru  wadau wake wote kwa kutoa ushirikiano kufanikisha zoezi la kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa wafungwa wa gereza la wilaya ya ileje mkoani Songwe.

‎‎Akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo,kaimu meneja wa kituo cha Redio Baraka chenye makao makuu yake mkoani Mbeya ndugu Sifael Kyonjola amesema lengo lilikuwa limekusudiwa limetimia.

kaimu meneja wa kituo cha Redio Baraka ndugu Sifael Kyonjola (picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya Kaimu meneja wa kituo cha Redio Baraka fm ndugu Sifael Kyonjola

‎‎Aidha mwenyekiti wa wadau bw.Christopher Sengo amesema wametoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwa ni pamoja na chakula, mashine za kunyolea,sabuni,mafuta pamoja na sukari.

Mwenyekiti wa wadau bw.Christopher Sengo (picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mwenyekiti wa wadau bw.Christopher Sengo

‎‎Kwa upande wake mchungaji kutoka idara ya magereza kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Stephano Ngondya amesema kila mtu anawajibu wa kutoa msaada kwa wahitaji.‎‎

Mchungaji kutoka idara ya magereza kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Stephano Ngondya(picha na Hobokela Lwinga)
Sauti ya mchungaji idara ya magereza kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi mch.Stephano Ngondya

Baadhi ya washiriki waliofika katika gereza la wilaya ya Ileje mkoani Songwe wamesema wao wameteleza wajibu wa kusaidia wahitaji kama ambavyo Mungu anavyoagiza kupitia Biblia Takatifu.‎‎

Sauti za baadhi ya wadau

Kituo hiki cha cha Redio Baraka kwa kushirikiana na wadau wake kimekuwa na utaratibu wa kila mwaka kuyaona na kutoa misaada kwa makundi mbalimbali ikiwemo, wazee, yatima na kutembelea wafungwa walioko magerezani