Baraka FM

Kada CCM ajitosa kuvaa viatu vya Dk Tulia Mbeya

24 May 2025, 15:29

Charles Mwakipesile picha na Ezra Mwilwa

Kuelekea uchaguzi Mkuu October 2025 baadhi ya makada kupitia vyama vyao vya siasa wameanza kutangaza nia zao kuwania nafasi mbalimbali ikiwemo udiwani,ubunge na urais.‎‎

Na Ezra Mwila ‎‎

Kada wa chama cha mapinduzi na mwandishi wa habari mkoani Mbeya Charles Mwakipesile ametangaza rasmi kugombea jimbo la Mbeya mjini Pindi mchakato utakapotangazwa.‎‎

Kada huyo ametangaza dhamira yake wakati akizungumza na wanahabari jijini Mbeya,amesema endapo atapewa ridhaa hiyo ataendeleza mazuri yote aliyo yaanzisha mbunge aliyepo Dkt.Tulia ambaye ametangaza kugombea jimbo la Uyole baada ya kugawanywa.‎‎‎

Charles Mwakipesile akizungumza na Wana habari(picha na Ezra Mwilwa)
Sauti ya Mwakipesile

Nao baadhi ya wananchi waliopo Jimbo la Mbeya mjini wamesema wanamshukuru Dkt Tulia kwa Utumishi wake hivyo wanaomba atakae pata nafasi ya kuongoza Jimbo Hilo aendeleze pale atakapoishia DKT Tulia Akson.‎‎

Sauti za wananchi waliopo jimbo la Mbeya mjini
Dkt. Tulia Akson akizungumza na nchi wa Jimbo la Uyole na Mbeya mjini Akitangaza kugombea jimbo jipya la Uyole(picha na Ezra Mwilwa)

Jimbo la Mbeya mjini limegawanywa na kupatikana kwa jimbo la Uyole ambalo Dkt.Tulia ametangaza rasmi kugombea katika nafasi ya ubunge.