Mpanda FM

SNV yarejesha tabasamu kwa wakulima

10 September 2026, 10:07 am

urejeshaji wa mto katika njia yake. Picha na Restuta Nyondo

“mashamba yangu yote yalikumbwa na mtaro wa maji”

Na. Restuta Nyondo

Wakulima katika Kijiji cha Mnyagala wamelishukuru shirika la SNV kwa kusaidia kurejesha mto katika njia yake na kuokoa mashamba yao ambayo yamekua yakipotea kila mwaka.

Wameiambia mpanda radio fm kuwa baadhi wamekuwa wakipoteza zaidi ya ekari 100 na kupoteza uzalishaji wa mazao kusombwa na maji baada ya mto huo kupoteza njia yake ya asili na kuwasababishia hali mbaya kiuchumi.

Sauti za wakulima mnyagala

Bruno Richard ni meneja mradi wa IKI KATUMA anayefanya kazi na SNV amesema kuwa mto huo ulihama njia kutokana na shughuli za kibinadamu ikiwemo kuchepusha maji hali iliyoathiri wakulima kwa kusababisha mafuriko kutokana na asilimia 60 ya maji yalikua yanaenda kwenye mashamba.

Sauti ya meneja mradi SNV

Aidha Mhandisi Almasi Mlala kutoka katika bonde la maji la ziwa Rukwa  amesema kuwa shughuli hiyo ya urejeshwaji wa mto katika njia yake ya asili kuna gharimu kiasi  kikubwa cha fedha na kuwataka wakulima kuacha tabia ya kuchepusha maji na kuwa walinzi wa mto huo na vyanzo vyote vya maji.

Sauti ya Mhandisi Mlala