Mpanda FM
Mpanda FM
22 April 2026, 2:18 pm

Wense Kamtoni diwani wa kata ya kashaulili. Picha na John Benjamin
“Biashara hii imeanzishwa kwa lengo la kutoa huduma kwa jamii na kukuza uchumi”
Na John Benjamin
Wawekezaji wameombwa kujitokeza kuwekeza katika nyanja ya kibiashara kata ya kashaulili iliyopo manispaa ya Mpanda mkoani Katavi
Hayo yamebainishwa na diwani wa kata ya kashaulili Wense Kamtoni katika ufunguzi wa Hela Supermarket iliyopo mtaa wa Simba ambapo ameeleza kuwa uwekezaji huo ni moja ya nyanja ya kukuza uchumi na kuahidi kuwaunga mkono wawekezaji
Kwa upande wake mmiliki wa Supermarket hiyo Herymathew Raymond amewakaribisha wananchi kufika na kupata huduma katika Supermarket hiyo huku akiahidi kutoa huduma bora Kwa wateja wataofika katika duka hilo
Kwa upande wao baadhi ya wananchi waliofika kushuhudia uzinduzi huo wamesema kuwa uwekezaji unaoendelea kuwekezwa katika mkoa wa Katavi umekuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo na wamempongeza mwekezaji huyo Kwa uwekezaji katika eneo hilo.
Uwekezaji katika maeneo mbalimbali ndani ya mkoa wa Katavi inatajwa kuwa moja ya jambo linalosaidia kukuza uchumi.