Mpanda FM
Mpanda FM
10 October 2025, 6:43 am

“Lengo ni kuwapenda watoto na kuwajali katika Bwana”
Na John Benjamin
Jamii mkoani Katavi imesisitizwa kutambua haki za watoto na kuhakikisha kuwa wanalelewa katika mazingira salama yenye heshima na upendo
Hayo yamebainishwa na mrakibu na Afisa wa jeshi la polisi jamii mkoa wa Katavi John Mwaipungu katika siku ya Mikaeli na watoto iliadhimishwa katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) lililopo Mpanda ambapo ameeleza aina mbalimbali za ukatili wanaofanyiwa watoto ikiwa ni pamoja na ukatili wa kimwili.
Kwa upande wao baadhi ya waumini wa kanisa hilo wameshukuru kwa elimu waliyopatiwa na kutoa wito kwa wazazi na walezi kuacha mara moja tabia ya kuwatumikisha watoto katika shughuli za biashara badala yake wawape nafasi ya kupata elimu na kufurahia utoto wao
Utoaji wa elimu hiyo ni sehemu ya kampeni ya Jeshi la polisi Jamii katika kupambana na vitendo vya kikatili dhidi ya watoto mkoani Katavi.