Mpanda FM

Tehama mkombozi kwa wananchi mahakamani

2 February 2026, 5:36 pm

Hakimu mkazi mfawidhi mahakama ya hakimu mkazi Katavi Gway Sumaye. Picha na Samwel Mbugi

Watu wanaweza kufungua kesi popote pale bila kufika mahakamani”

Na Samwel Mbugi

Mahakama nchini Tanzania imefanikiwa kufanya maboresho ya mifumo ya tehama na kurahisisha upatikanaji huduma za uendeshaji wa kesi kwa njia ya mtandao kama utekelezaji wa dira ya upatikanaji wa  haki sawa kwa wote kwa wakati. 

Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Katavi, Gway Sumaye amesema maadhimisho hayo  ni kiashiria cha kuanza kazi kwa mwaka kwa kupokea mashauri na kuyatolea maamzi kwa wakati.

Hakimu mkazi mfawidhi

Akizungumza mbele ya mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ambae amemwakilisha mkuu wa mkoa wa katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko ameipongeza mahakama kwa kuboresha huduma ikiwemo matumizi ya tehama pamoja na miundombinu ya mahakama hiyo.

Mkuu wa wilaya

Awali akisoma tarifa mbele ya mgeni rasmi mwendesha mashitaka mkoa wa Katavi amesema maadhimisho hayo yanakumbusha dhima na wajibu wa pamoja katika kulinda amani na haki ya kila mwananchi.

mwendesha mashtaka

Maadhimisho ya mwaka huu kitaifa yamefanyika jijini Dodoma yakiwa yamebeba kauli mbiu isemayo mchango wa Mahakama katika ustawi na maendeleo ya taifa.