Daraja la Msadya lakamilika, laanza kutoa huduma kwa wananchi Katavi
12 December 2023, 10:10 am
Picha na Site Tv
Daraja hilo limegharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 4.8
Na Betord Benjamini-Katavi
Daraja la Msadya lenye urefu wa Mita 60 lilipo katika halmashauri ya Mlele mkoani Katavi limekamilika na limeanza kutoa huduma kwa wananchi.
Akizungumza Meneja wa TARURA wilaya ya Mlele Mhandisi Paul Mabaya amesema daraja hilo limegharimu kiasi cha shilingi bilioni 4.8 na kuahidi kuendelea kutekeleza miradi kwa ufanisi ili pesa zinazotolewa na serikali ziweze kuwanufaisha wananchi.
Picha na Site Tv
Awali wakizungumza wananchi pamoja na baadhi ya madiwani wa halmshauri hiyo wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kukamilisha ujenzi wa daraja hilo kutokana na usumbufu waliokuwa wanakabiliano nao. .