Mpanda FM

Wananchi Katavi watakiwa kuchukua vitambulisho vya taifa

4 April 2024, 8:45 pm

Afisa  Msajili  mamlaka ya vitambulisho vya taifa  wilaya ya Mpanda Mauna Karumbeta akiwa katika Studio za Mpanda Redio Fm .Picha na Anna Milanzi

Amewataka wananchi kuthamini juhudi za serikali kwa kufika kuchukua vitambulisho na kuvitunza kwani serikali imetumia gharama

Na Lilian Vicent -Katavi

Wito umetolewa kwa Wananchi wa mkoa wa Katavi   ambao hawakupata Vitambulisho vya NIDA kufika  Ofisi   za Mitaa Wanayoishi  ili kuweza kuvichukua  kabla havijarudishwa Ofisi   za NIDA .

 Hayo yamesemwa na Afisa  Msajili  Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa  Wilaya ya Mpanda Mauna Karumbeta Wakati akizungumza na Mpanda Redio Fm na kueleza   kuwa kuna baadhi ya Kata Vitambulisho vya awamu ya kwanza bado vipo mpaka sasa Wananchi hawajavichukua.

Sauti ya Afisa  Msajili  mamlaka ya vitambulisho vya taifa  wilaya ya Mpanda Mauna Karumbeta

Nae   Afisa usajili Tanganyika Zainabu Mwinyimvua amewataka wananchi kuthamini juhudi za serikali kwa kufika kuchukua vitambulisho na kuvitunza kwani Serikali imetumia gharama.

Sauti ya Afisa usajili Tanganyika Zainabu Mwinyimvua

Afisa usajili Tanganyika Zainabu Mwinyimvua akiwa katika Studio za Mpanda Redio Fm .Picha na Anna Milanzi

Kwa upande wao wananchi wamesema kuwa vitambulisho hivyo vitawasaidia  kwani wamesubiri kwa muda mrefu na ili wakwamisha kupata baadhi ya huduma  zinazohitaji vitambulisho.

Sauti za Wananchi Mkoani Katavi wakishukuru kuletewa vitambulisho hivyo