Mpanda FM

Dawati Katavi kusimama na wanafunzi

24 October 2023, 4:08 am

Mkuu wa Dawati Mkoa wa Katavi Judith Mbukwa akitoa elimu kwa wanafunzi Magamba. Picha na Festo Kinyogoto

Dawati la jinsia na watoto Katavi laahidi Kuwalinda wanafunzi ili waweze kutimiza Ndoto Zao.

Katavi
Kitengo cha Dawati la jinsia na watoto Mkoani Katavi Kimewahakikishia Kuwalinda wanafunzi Dhidi ya mienendo Mibovu ili waweze kutimiza Ndoto Zao.

Akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari Magamba katika mwendelezo wa kutoa elimu Mkuu wa kitengo cha dawati la jinsia na watoto mkoa wa Katavi Judith Mbukwa amewataka wanafunzi kuepuka makundi yanawapelekea kujiingiza katika makundi ya kiuhalifu, mapenzi katika umri mdogo na kutaka kuzingatia masomo.

Sauti ya Judith Mbukwa
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Magamba wakimsikiliza Mkuu wa Dawati Katavi. Picha na Festo Kinyogoto

Kwa upande wa wanafunzi wa shule ya Sekondari Ya Magambawakizungumza kuhusu elimu waliyopatiwa wameahidi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kutoa taarifa kuhusu matukio ya kiukatili wanayofanyiwa ili waweze kutimiza ndoto zao.

Sauti za Wanafunzi

Dawati la Jinsia Tanzania ni kitengo maalumu ndani ya jeshi la polisi  kinachoshughulikia kesi na matukio ya ukatili dhidi ya watoto.