Mpanda FM

Zimamoto Katavi yaadhimisha siku yao kwa kutoa elimu

4 May 2026, 6:36 pm

Jeshi la zimamoto likiadhimisha siku yao. Picha na Roda Elias

“Nitoe rai msipende kupambana na tukio la moto wenyewe”

Na Roda Elias

Jeshi la zimamoto mkoani Katavi limetoa elimu kwa wananchi kuhusiana na majanga yatokanayo na mvua zinazoendelea kunyesha, kwa baadhi ya maeneo na majanga ya moto yanayotokana na ajali.

Hayo yamejiri kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya zimamoto duniani, maeneo ya Mpanda hotel manispaa ya Mpanda mkoani Katavi Lilian Wanna, kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto mkoani Katavi amesema kuwa jamii haipaswi kujichukulia maamuzi ya kupambana na majanga hususani majanga ya moto badala yake wanapaswa kutoa taarifa kwa jeshi hilo ili kufanikisha uokozi.

Sauti ya kaimu kamanda

Kwa upande wa baadhi ya wananchi waliohudhuria katika utolewaji wa elimu hiyo wameeleza namna ambavyo wameipokea elimu hiyo huku wakiliomba jeshi hilo kuendelea kutoa elimu hiyo mara kwa mara.

Sauti za wananchi

Siku ya zimamoto duniani huadhimishwa kila mwaka mnamo tarehe 4 mwezi wa 5 ambapo mwaka huu mkoani katavi jeshi hilo limedhimisha kwa kufanya matembezi kwa baadhi ya maeneo katika manispaa ya Mpanda.