Mpanda FM

Darasa la saba ndani ya chumba cha mtihani Septemba 10

9 September 2025, 8:41 pm

Leonard Victor afisa elimu manispaa ya Mpanda.Picha na Sumaiya Emmanuel

“Nimejiandaa vizuri na nafurahi kuhitimu elimu yangu ya msingi”

Na Sumaiya Emmanuel

Jumla ya wanafunzi  5312 wanatarajiwa kufanya mitihani ya kumaliza elimu ya msingi manispaa ya Mpanda mkoani Katavi.

 Akizungumza na Mpanda radio FM afisa elimu manispaa ya Mpanda Leonard Victor Rutta amesema maandalizi ya awali kuelekea mtihani huo yamekamilika  na kueleza manispaa imeshakamilisha mipango kuelekea ufanyikaji wa mitihani hiyo.

Sauti ya afisa elimu manispaa ya Mpanda

 Kwa upande wao Wanafunzi wa baadhi ya shule za msingi manispaa ya Mpanda wamesema maandalizi kuelekea mitihani yao yamekamilika na kuwaahidi wazazi na walimu kufanya vizuri katika mitihani hiyo.

Sauti ya wanafunzi

Kwa upande wao, baadhi ya wazazi wamesema wamekuwa wakishirikiana kwa karibu na walimu pamoja na  kuwaandaa  watoto kisaikolojia ili kuondoa hofu na kuongeza hali ya kujiamini. Wameeleza kuwa motisha na malezi ya karibu ni silaha kubwa ya kuwasaidia watoto kufanikisha mtihani.

Sauti za wazazi