Mpanda FM

Mbwa waleta gumzo ,wamiliki watajwa

29 June 2026, 3:13 pm

Juu kushoto, ni daktari Mundhiri Bashiri wa hospitali ya manispaa ya Mpanda, Kulia juu ni daktari wa mifugo halmashauri ya manispaa ya Mpanda Eward Mtega. Picha na Anna Milanzi

“Kumekuwa na mbwa wanaodhurura ovyo hawana uangalizi kutoka kwa wamiliki hali inayozua hofu “

Na Anna Milanzi- Katavi

Wakazi manispaa ya Mpanda   mkoani Katavi wamewasisitiza wamiliki wa mbwa kufungia mbwa wao ili kuwaepusha na ugonjwa wa kichaa cha mbwa  ambao mtu anaupata baada ya kung’atwa na mbwa mwenye maambukizi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi hao akiwemo Happynes Samwel, Nicolaus Luwele, Sesilia Sangu wamesema kuwa kumekuwa na mbwa wanaodhurura ovyo hawana uangalizi kutoka kwa wamiliki hali inayozua hofu kwa wakazi hao hasa kupata kichaa cha mbwa endapo mtu kang’atwa na mbwa mwenye maambukizi.

Sauti za wakazi wa manispaa ya Mpanda

 Daktari wa mifugo wa halmashauri ya manispaa ya Mpanda Eward Mtega ameeleza visa vilivyoripotiwa vya watu waliong’atwa na mbwa.

Sauti ya daktari wa mifugo Eward mtega

Amesema zipo hatua wanazozichukua endapo wakipata taarifa za mtu kung’atwa na mbwa.

Sauti ya Eward mtega daktari wa mifugo halmashauri ya manispaa ya Mpanda

Mratibu wa huduma za  matibabu hospitali ya manispaa ya Mpanda Daktari  Mundhiri  Bashiri amewataka wananchi wanaong’atwa na mbwa kufika haraka katika kituo cha kutolea huduma za afya ili waweze kupatiwa matibabu.

Sauti ya mratibu wa huduma za matibabu hospitali ya manispaa ya Mpanda Mundhiri Bashiri.

Hata hivyo wamiliki wa mbwa wamekumbushwa kuwafungia mbwa wao na kuwapatia chanjo  ili kudhibiti  madhara kwa binadamu .