Mpanda FM
Mpanda FM
10 October 2024, 4:18 pm

Wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi ametoa maoni mseto kuhusiana na sababu zinazopelekea wazazi na walezi kuwafanyia ukatili watoto wao.
Wakizungumza na Mpanda Radio FM wananchi hao wamesema kuwa ukosefu wa elimu na malezi duni imekuwa ni sababu kubwa zinazopelekea watoto kufanyiwa ukatili
Nae mkaguzi wa polisi Judith Mbukwa ambaye ni mkuu wa dawati la jinsia na watoto mkoa wa katavi amethibitisha kuwa wazazi wengi wamekuwa wakiwafanyia ukatili watoto wao kutokana na imani za kishirikina pamoja na umaskini hivyo amewasihi wazazi kuwa na ushirikiano na jeshi la polisi katika kutokomeza ukatili dhidi ya watoto
Ikumbukwe kuwa sheria ya mtoto inazuia mtoto kufanyiwa ukatili, unyama pamoja na vitendo visivyo vya kibinadamu au udhalilishwaji unaohusisha matendo ya kimila yanayoondoa utu wa mtu au kuathiri ustawi wa akili na maumbile yake.