Mpanda FM

Matembezi ya TRA Katavi  yaongeza nguvu usafi wa mazingira

27 June 2026, 6:13 pm

Lengo la kufanya hivyo ni kuchangia kuuweka mkoa katika hali ya usafi

Na Anna Milanzi -Katavi

Katika kuendelea na maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya mapato Tanzania  (TRA) ,TRA mkoa wa Katavi imekuja na suluhisho la uhifadhi wa taka na kuweka hamasa ya usafi wa mazingira.

Katibu tawala mkoa wa Katavi aliyevaa kofia nyeupe, kushoto kwake ni kaimu meneja wa TRA mkoa wa Katavi , kulia kwake ni kaimu mkurugenzi manispaa ya Mpanda pamoja na wadau wengine.

Akizungumza katika uwanja wa azimio mara baada ya kukamilika kwa matembezi ya kilometa 5 kaimu meneja wa TRA mkoa wa Katavi Joshua Mile amesema lengo la kufanya hivyo ni kuchangia kuuweka mkoa katika hali ya usafi huku akieleza mapipa zaidi ya 25 yanatarajiwa kuwekwa katika maeneo ya mji wa Mpanda.

Sauti ya kaimu meneja wa TRA mkoa wa Katavi Joshua Mile

Akimwakilisha mkurugenzi wa manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli, Gwalusajo Kapande amesema mapipa ya taka yatasaidia kuweka mji safi ambapo amewasisitiza wananchi pia kulipa kodi ili kuleta maendeleo

Sauti ya kaimu mkurugenzi manispaa ya Mpanda

Katibu tawala mkoa wa Katavi  Albert Msovela amesema TRA imepiga hatua katika ukusanyaji wa mapato kwa kuvuka malengo waliyojiwekea.

Sauti ya Katibu tawala mkoa wa Katavi

Nao baadhi ya wananchi akiwemo Khadija Mtalika na Izack Joseph waliohudhuria matembezi hayo wamepongeza kazi zinazofanywa na mamlaka ya mapato Tanzania ( TRA )na kusisitiza wananchi wengine kulipa kodi.

Sauti ya wakazi wa mkoa wa Katavi

Miongo mitatu ya TRA  Katavi, jamii inaendelea kupata elimu juu ya umuhimu wa kulipa kodi.