Mpanda FM
Mpanda FM
18 June 2026, 11:55 am

“wanafanya ukaguzi huo wakati huu walikizo ili shule zitakapofunguliwa magari hayo yawe yana usalama wa kubeba wanafunzi huku akisema hatua za kisheria zitachukuliwa kwa ambao watakiuka agizo hilo“
Na Anna Milanzi-Katavi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Katavi amewahimiza wamiliki wa mabasi ya shule mkoani katavi kuyapeleka mabasi hayo kufanyiwa ukaguzi.
Akizungumza mara baada ya kufanyika kwa ukaguzi wa mabasi hayo kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Kaster Ngonyani ambaye ni kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Katavi amesema wamekagua magari 24 na kubaini mapungufu katika magari mawili.
Kamanda Ngonyani amesema wanafanya ukaguzi huo wakati huu walikizo ili shule zitakapofunguliwa magari hayo yawe yana usalama wa kubeba wanafunzi huku akisema hatua za kisheria zitachukuliwa kwa ambao watakiuka agizo hilo
Akizungumza kwa niaba ya jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Katavi askari wa jeshi hilo Frank Omwagore amewashauri wamiliki wa magari kuhakikisha magari yao yanakuwa na vizimia moto
Kwa upande wao madereva na walezi wa wanafunzi katika magari hayo wamepongeza hatua hiyo ya ukaguzi na kuwakumbusha wengine kuzingatia usalama wa watoto.
Zoezi hilo la ukaguzi linafanyika kwa siku tatu ambapo limeanza june 17, 2026