Mpanda FM
Mpanda FM
8 August 2024, 9:28 am

Picha na Mtandao
“kupima afya ya mwili mara kwa mara kunasaidia kuondoa usugu wa magonjwa kwani kama ukibainika kuwa na ugonjwa unatibiwa katika hatua za awali za ugonjwa”
Na Rachel Ezekia-Katavi
Baadhi ya wananchi wa manispaa ya mpanda mkoani Katavi wametoa maoni mseto kuhusiana na umuhimu wa kuchunguza afya ya miili yao mara kwa mara ili kufanya shughuli za kimaendeleo kwa ufanisi
Wameyasema hayo walipokuwa wanazungumza na Mpanda Radio FM ambapo wameeleza kuwa watu wengi wamekuwa hawafanyi hivyo kutokana na hofu endapo wakibainika kuwa na magonjwa.
sauti za wananchi wakitoa maoni yao
Daktari Paulo Lugata ambaye pia ni mganga mfawidhi wa hospitali ya manispaa ya Mpanda ameeleza kuwa kufanya uchunguzi wa mwili au body chekup kunasaidia kugundua viashiria vya ugonjwa mapema na kutafutia ufumbuzi .
Sauti daktari akizungumzia umuhimu wa kufanya checkup ya mwili
Katika hatua nyingine daktari lugata amesema wananchi wengi wamekuwa wakifika hospitali mpaka wanapoumwa na sikwenda kwa hiari kuchunguza miili yao.
sauti ya daktari akizungumzia mwenendo wa wananchi kwenda hospitali hadi wanapoumwa
Ameongeza kuwa ni rahisi kutibu ugonjwa ukiwa katika hatua za mwanzo kwani magonjwa mengi hayaonyeshi dalili kwa haraka.