Mpanda FM

TAG Katavi yakita kambi kuombea maadili kwa vijana

30 April 2026, 2:06 pm

Kushoto ni katibu msaidizi idara ya vijana jimbo la Katavi Magharibi Mwl Semeni Lusekelo. Picha na Anna Mhina

“Kijana aliyeokoka akikosa maadili ya kiroho anakosa uaminifu”

Na Anna Mhina

Uongozi wa kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) section ya Kabungu iliyopo kata ya Kabungu wilayani Tanganyika mkoani Katavi wamefanya kambi la maombi ya siku tatu kwa ajili ya kuombea maadili kwa vijana.

Akizungumza na Mpanda Radio FM wakati wa kufunga kambi hilo lililoamabatana na ziara ya viongozi wa jimbo, katibu msaidizi wa idara ya vijana jimbo la Katavi Magharibi Semeni Lusekelo ameeleza sababu za kufundisha somo la maadili kwa vijana ni kuwafanya wawe waaminifu hata wanapopata nafasi za uongozi serikalini.

Sauti ya katibu msaidizi Jimbo la Katavi

Kwa upande wake mkurugenzi wa vijana section ya Kabungu mchungaji Lameck Garidi ameeleza lengo la kufanya kambi la maombi kwa vijana  ni ili waweze kurejea katika misingi bora,  kuwajengea hofu ya Mungu pamoja na kuishi maisha yenye maadili mema.

Sauti ya mkurugenzi section ya Kabungu

Nao baadhi ya vijana waliohudhuria kambi hilo la maombi wameahidi kuyaishi yale yote waliyofundisha na kutarajia maombi hayo yataleta mabadiliko makubwa kwao, katika jamii na taifa kwa ujumla.

Sauti za vijana

Kambi hilo la maombi ya siku tatu limefanyika katika kijiji cha Kamsenga kilichopo kata ya Kabungu wilaya ya Tanganyika na kuhudhuriwa na makanisa kumi likiwemo kanisa la Mchakamchaka, Majalila, Ifinsi, Bugwe, Kabatini, Kibo, Kamsenga, Silonge, Kasinde pamoja na kanisa la Kambanga.