Mpanda FM

Shughuli za utafutaji zinavyochangia utelekezaji wa familia

28 September 2023, 12:09 am

Picha na Mtandao

Wazazi na walezi mkoani Katavi wameaswa kuachana na tabia ya kusafiri kwa lengo la kufanya shughuli za utafutaji na kutelekeza familia

Na William Liwali – Katavi

Wazazi na walezi mkoani Katavi wameaswa kuachana na tabia ya kusafiri kwa lengo la kufanya shughuli za utafutaji na kutelekeza familia hali inayosababisha watoto wengi kujiingiza katika vishawishi na kuharibikiwa kimaisha.

Changamoto wanazopitiawatoto hao ni pamoja na kukosa muda wa masomo lakini pia kushindwa kuhimili baadhi ya vishawishi kutoka kwa watu wanaowazunguka kulingana na hali ngumu ya uchumi wa familia.

Wito huo umetolewa na inspekta Kelvin Fuime kutoka kitengo cha polisi jamii na dawati la jinsia na watoto mkoa wa Katavi na Kuainisha madhara yanayoweza kujitokeza endapo watoto wataishi wenyewe bila uangalizi wa wazazi.

Sauti ya Inspekta Kelvin Fuime

Nao baadhi ya watoto wameeleza changamoto wanazopitia ikiwa ni pamoja na kukosa muda wa masomo lakini pia kushindwa kuhimili baadhi ya vishawishi kutoka kwa watu wanaowazunguka kulingana na hali ngumu ya uchumi wa familia.

Sauti ya baadhi ya watoto

Kwa upande wa baadhi ya wazazi wamelitazama swala hilo katika mtazamo hasi na kusema kuwa yapo madhara ikiwemo kushindwa kujisimamia katika misingi bora na kuangukia katika makundi yasiyofaa kutokana na uhuru walionao kwa wakati huo.

Sauti ya baadhi ya wazazi