Mpanda FM

Rais wa chemba ya wafanyabiashara nchini azitaka taasisi binafsi kuungana

19 April 2024, 11:41 pm

Rais wa chemba  ya wafanyabiashara Tanzania [TCCIA] Vicent Bruno Minja akizungumza na wafanyabiashara mkoani Katavi.Picha na Veronika Mabwile

changamoto zinashindwa kutatuliwa kutokana na wafanyabiashara wenyewe kutokuwa na umoja

Na Veronika Mabwile -Katavi

Rais wa chemba  ya wafanyabiashara Tanzania [TCCIA] Vicent Bruno Minja amezishauri  Taasisi binafsi Mkoani Katavi  kuungana ili kusaidia kuongeza uzito kwa serikali katika kutatua  changamoto zinazo zikabili taasisi hizo .

Ushauri huo ameutoa  wakati wa kikao na wafanyabiashara kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda na kusema kuwa changamoto zinashindwa kutatuliwa kutokana na wafanyabiashara wenyewe kutokuwa na umoja

Sauti ya Rais wa chemba  ya wafanyabiashara Tanzania [TCCIA] Vicent Bruno Minja

Kwa upande wao wafanyanyabiashara waliohudhuria kikao hicho wamezitaja changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo miundombinu mibovu ya barabara ambayo wamesema inachangia ucheleweshwaji wa mizigo 

Sauti ya wafanyanyabiashara waliohudhuria kikao hicho wakitaja changamoto mbalimbali zinazowakabili

Viongozi wa  Chemba ya biashara Mkoani hapa wamesema kuwa wanamkakati wa kuanzisha dawati la kikodi kwa lengo la kuwasaidia wafanyabiashara kutatua changamoto zitokanazo na malipo ya kodi.

Sauti ya Viongozi wa  Chemba ya biashara Mkoani Katavi

Rais wa chemba ya wafanyabiashara hapa nchini anafanya ziara ya kutembelea mikoa yote 26 ya Tanzania Bara kwa lengo la kusikiliza kero na kutazama fursa zilizopo katika mikoa hiyo.