Mpanda FM

Dkt. Nchimbi apokelewa Katavi kwa kishindo

13 April 2024, 11:18 pm

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa Dkt.Emmanuel Nchimbi akiwasili Katika uwanja wa ndege Mkoani Katavi kwa ajili ya ziara ya siku mbili Mkoani hapa .Picha na Samwel Mbugi

Amewataka Viongozi kuhakikisha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Wanaweka Wagombea ambao wanajiuza kwa Wananchi na sio kuweka Wagombea watakaotakiwa kusafishwa

Na Samwel Mbugi -Katavi

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa Dkt.Emmanuel Nchimbi na Wajumbe wake,Wamewasili Mkoani Katavi kwa Ziara ya Siku mbili.

Dkt. Nchimbi ameongozana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa,itikadi,uenezi na Mafunzo Amos Makalla na Katibu wa NEC, Organization Issa Ussi Haji Gavu.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa Dkt.Emmanuel Nchimbi akisalimiana na Viongozi mbalimbali wakati wa Mapokezi yake.Picha na Samwel Mbugi

Akizungumza katika maeneo ya Viwanja vya CCM Mkoa, Issa Ussi Gavu amewataka Viongozi kuhakikisha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Wanaweka Wagombea ambao wanajiuza kwa Wananchi na sio kuweka Wagombea watakaotakiwa kusafishwa

Sauti ya Katibu wa NEC, Organization Issa Ussi Gavu akizungumza na kuwataka Viongozi wa CCM mkoa wa Katavi wanawaweka Wagombea wanaostahili

Kwa upande wake Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, itikadi, Uenezi na Mafunzo Amos Makalla amesema kuwa utaratibu utakaotumika kusikiliza kero za Wananchi ni zile ambazo hazipo Mahakamani.

Sauti ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Amos Makalla akizungumza

Dkt. Nchimbi ametoa salamu za Chama katika Ofisi za CCM mkoa wa Katavi ambapo amewashukuru Viongozi wa Serikali na Chama kwa kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Sauti ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa Dkt.Emmanuel Nchimbi akizungumza na kuwashukuru Viongozi wa Serikali na Chama

Dkt. Nchimbi ameteuliwa January 15 Mwaka huu kupitia kikao cha Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Kilichoketi Visiwani Zanzibar kikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dkt. Samia Suluhu Hassan.