Mpanda FM
Mpanda FM
10 October 2024, 5:17 pm

picha na mtandao
“Wanatozwa pesa kiasi cha shilingi 200 kwa kila mwananafunzi kila siku”
Na Leah Kamala -Katavi
Baadhi ya wazazi na walezi wanaosomesha watoto wao katika shule ya msingi Muungano ,manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamelalamikia suala la mchango hasa kwa masomo ya muda wa ziada.
hatua hiyo imekuja baada ya baadhi ya watoto kusoma masomo ya ziada katika shule hiyo huku wazazi hao wakidai kuwa wanatozwa pesa kiasi cha shilingi 200 kwa kila mwananafunzi kila siku
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wazazi hao wamewaomba walimu hao kuwa wafute masomo ya ziada na ubaki muda wa unaojulikana na serikali .
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Teresia Peter Kijika amekanusha suala la wanafunzi kudaiwa pesa ya masomo ya ziada (TWISHENI) Na kuongeza kuwa kazi ya ualimu ni wito hivyo wao walimu wanajitoa kwa moyo kuhakikisha watoto wanafanya vizuri katika masomo yao.
Sauti ya mwalimu mkuu akizungumzia suala hilo
Aidha mwalimu huyo amebainisha faida za kuwepo na masomo rekebishi kwa watoto hivyo wazazi waweke nguvu katika kuwasimamia watoto wao.
Sauti ya mwalimu mkuu akizungumza
Naye peter chandalala ambae ni mwenyekiti wa shule hiyo amesema kuwa wazazi wengi hawazungumzi na watoto wao pindi wanaporudi nyumbani hali inayopelekea wazazi kutokuelewa nini kinaendelea shuleni.
Mwenyekiti wa kamat i ya shule akieleza