Mpanda FM
Mpanda FM
20 May 2026, 3:05 pm

Na Anna Milanzi-Katavi
Wakulima mkoani Katavi wameshauriwa kutumia mizani katika mauzo ya mazao na kuachana na Vipimo batili.
Katika kuadhimisha siku ya vipimo duniani meneja wakala wa vipimo mkoa wa Katavi Mrinde Elihaki amewashauri wakulima kuzingatia matumizi ya vipimo halali na kuacha kukubaliana na vipimo visivyo rasmi
Ameyasema hayo alipokuwa katika kipindi cha kumekucha Tanzania kinachorushwa kupitia Mpanda redio FM may 20, 2026.
Kufuati uwepo wa siku hii, wananchi mkoani Katavi wametoa ombi kwa wakala wa vipimo mkoa wa Katavi kuhakikisha elimu inatolewa kwa wananchi ili waweze kutambua umuhimu wa kutumia Vipimo ikiwemo mizani.
Kaulimbiu ya mwaka huu inasema sayansi ya vipimo isaidie kujenga imani katika utungaji wa sera .