Mpanda FM

Katavi :Wafanyabiashara walia na umeme

8 August 2024, 9:51 am

picha na mtandao

“kukatika kwa umeme mara kwa mara kunasababisha kushuka kiuchumi ambapo wafanyabiashara hao wanajikuta wanakuwa na kipato duni”

Na John Benjamin- Katavi

Wafanyabiashara manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamelalamikia adha ya kukatika kwa umeme mra kwa mara hali ambayo inawasababishia hasara

Hayo yamebainishwa na wafanyabiashara wakati wakizungumza na Mpanda Redio FM kwa nyakati tofauti na kueleza kuwa  Uchumi wao unayumba kutokana na shughuli zao kuhitaji umeme.

Sauti ya wafanyabiashara wakizungumza juu ya changamoto ya umeme

Akizungumza kwa njia ya simu afisa mahusiano wa shirika la umeme Tanzania mkoa wa Katavi Proches Joseph amesema kuwa kumekuwa  na maboresho kwa baadhi ya laini ya nishati hiyo  ya umeme.

Sauti ya afisa mahusiano wa shirika la umeme Tanzania mkoa wa katavi Proches Joseph

Kwa mujibu wa taarifa hiyo maboresho yanayofanyika  ni kwa ajili ya maandalizi ya mapokezi ya umeme wa  gridi ya taifa mwezi ujao