Mpanda FM
Mpanda FM
7 July 2025, 7:34 pm

Wajasiriamali wakiwa kwenye mafunzo. Picha na Anna Mhina
“Lengo ni kuhakikisha wanakatavi wanapata mafunzo ya uchumi na ujasiriamali”
Na Anna Mhina
Zaidi ya wajasiriamali 80 mkoani Katavi wamepatiwa mafunzo ya namana ya ufugaji bora wa kuku, utengenezaji wa sabuni pamoja na utengenezaji wa batiki.
Akizungumza na Mpanda radio FM mwalimu Benjamin Chahe kutoka chuo cha Mkwawa V.T.C kilichopo Iringa ameeleza lengo la kufanya mafunzo hayo ni kuwakwamua kiuchumi wananchi wa katavi.
Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wameeleza namna walivyonufaika na mafunzo hayo na kuahidi kuyatendea kazi ili kuweza kujikwamua kiuchumi.
Mafunzo hayo yameandaliwa na Mpanda radio FM kwa kushirikiana na chuo cha Mkwawa VTC kilichopo Iringa mjini ambapo yatafanyika kwa siku tatu katika ukumbi wa CCM wilaya ya Mpanda.