Mpanda FM
Mpanda FM
7 September 2026, 2:56 pm

Na. Ben Gadau
“Wananchi wasibeze taarifa zinazotolewa na mamlaka ya hali ya hewa“
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamil Yusuph Kimaro, amewataka wananchi kuchukua tahadhari mapema ili kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua za El-Nino zinazotarajiwa kuanza hivi karibuni.
Akizungumza katika kipindi cha Kumekucha Tanzania, DC Jamila amewataka wananchi wanaoishi maeneo ya mabondeni na maeneo hatarishi kuchukua hatua mapema, ikiwemo kuhama maeneo hayo na kwenda sehemu salama, ili kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na mafuriko na kujaa kwa maji.
Aidha, Jamila amewataka wananchi kuwa makini katika maeneo ya migodi, mito na maeneo mengine hatarishi, huku akisisitiza umuhimu wa kusafisha mifereji ya maji na kuzingatia taarifa na maelekezo yanayotolewa na mamlaka.
DC Jamila amesema maandalizi ya mapema ni muhimu katika kulinda maisha, mali na shughuli za wananchi wakati wa msimu huo wa mvua.