Nuru FM
Nuru FM
13 February 2026, 10:12 am

Mpango huu umekuja ili kuhakikisha wananchi wapata huduma za afya bila vikwazo.
Na Joyce Buganda
Wananchi 7827 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Iringa yenye kata 28 wamashatambuliwa na wanatarajiwa kunufaika na mpango wa bima kwa wote kampeni ambayo inaendelea nchi nzima yenye lengo la kuhakikisha wananchi wanapata huduma za matibabu pasipo vikwazo vya kifedha.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi la uhakiki, usajili na ugawaji wa bima za afya kwa wote wasio na uwezo lililofanyika katika kijiji na kata ya kisin’ga Wilayani Iringa Mratibu wa bima ya afya kutoka Halmashauri ya Iringa Dkt Renatha Kato amesema halmashauri ya wilaya hiyo inaanza zoezi hilo kwa awamu ya kwanza ambayo wameanza na watu wasiojiweza makundi maalumu kama watu wenye ulemavu, Wazee, wajawazito na watoto ambayo kwa awamu hii watagharamiwa na serikali.

Awali Afisa Tarafa Kutoka Tarafa ya Ismani Benitho Kayugwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Iringa amesema serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania imeona wananchi wake wanavyopata tabu hasa katika sekta ya kiafya na wameanza na makundi maalumu ambao watapata kadi za bima ya afya ambayo watapata matibabu bure, huku akiendelea kuwasisitiza wananchi hao kuzitunza kadi hizo,
Nao baadhi ya wanufaika wa Mpango wa Bima ya afya kwa wote wameishukuru serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuwapatia kadi hizo huku wakisema mwanzoni walikuwa wakishindwa kwenda kutibiwa kutokana na ghalama kubwa za matibabu.
Ikumbukwe kuwa mpango wa bima ya afya kwa wote ni mpango wa Taifa ambao unalenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma za matibabu bila kuathiriwa na ghalama kubwa ambapo kwa wale wanaolilipia watatakiwa kulipia shilingi 150,000 ambayo itajumuisha watu 6 katika kaya.
