Nuru FM

EAMCEF kuwafadhili wakulima na wafugaji Iringa

28 January 2026, 5:30 pm

Wanufaika wa Mfuko wa EAMCEF. Picha na Joyce Buganda

Na Joyce Buganda

Serikali mkoani Iringa imeanzisha Mfuko wa Uhifadhi wa Milima ya Tao la Mashariki EAMCEF unaolenga kufadhili wakulima na wafugaji katika jitihada za uhifadhi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Hayo yamezungumzwa na Afisa  mazingira mkoani Iringa Golyama Bahati na kuongeza kuwa kuna vigezo vinavotumika ni  wakulima na wafugaji kutengeneza vikundi ili kuwafikia kwa urahisi.

Sauti ya Goliama

Kwa upande wao Wanufaika wa mradi wa EAMCEF wanasema wamefaidika, ikiwemo kupata bayo-gesi inayosaidia katika kilimo na ufugaji.

Sauti ya Wanufaika

Naye Afisa Mifugo Mkoa wa Iringa Bw. Chacha Mwita anatoa wito kwa wafugaji kuacha kufuga kwa mazoea badala yake wapende kuijfunza  vitu vipya.

Sauti ya Afisa Mifugo

Mabadiliko ya tabianchi ni changamoto kubwa kwa Wakulima na wafugaji  hivyo wanahitaji mikakati thabiti, shirikishi, na uwajibikaji wenye tija.