Nuru FM

Muyinga: Watoto wenye ulemavu wapelekwe shule

15 January 2026, 12:22 pm

Mkurugenzi wa kituo kinachotoa huduma za utengamao mkoani Iringa cha Lebao’s Kids Foundation Theophil Muyinga akizungumza. Picha na Joyce Buganda

Kundi la watoto wenye ulemavu linapaswa kupata elimu kama watoto wengine.

Na Joyce Buganda

Wazazi na walezi  wenye watoto wenye ulemavu mkoani Iringa wameshauriwa kuwapeleka watoto wao waliofikiwa umri wa kwenda shule Ili kupata haki ya msingi na kufikia ndoto zao.

Ushauri huo umetolewa umetolewa  na Mkurugenzi wa kituo kinachotoa huduma za utengamao mkoani Iringa cha Lebao’s Kids Foundation Theophil Muyinga wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake na kusema kuwa wazazi wasikate tamaa kuona wamepata watoto au mtoto mwenye ulemavu hivyo wawape haki za msingi kama elimu.

Sauti ya Muyinga

Aidha  Muyinga amewasihi wazazi wasikate tamaa kuona wana watoto wenye ulemavu kwani wanauwezo wa kufanya shughuli mbalimbali pia  kuwasaidia kuwainua kwa pamoja.

Sauti ya Muyinga

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa chama cha watu wenye Ualbino nchini Alfred kapole amewataka wazazi kuhakikisha watoto wenye ulemavu wa ualbino wanawapeleka watoto wao kupata elimu kwani usalama upo kila sehemu.

Sauti ya Kapole

Hayo yamekuja kutokana na baadhi ya  wazazi kuwaficha watoto wenye ulemavu na kutowapa haki zao za kimsimgi ikiwemo elimu.