Nuru FM

MTAKUWWA kutokomeza ukatili kwa vitendo Iringa

26 November 2025, 10:46 am

Wadau wa ukatili katika picha ya pamoja. Picha na Joyce Buganda

Matukio ya ukatili yamekuwa yakidumaza ustawi wa watoto na wanawake.

Na Joyce Buganda

Wadau na Wajumbe wa mpango wa Taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto MTAKUWWA sehemu ya 2 wametakiwa  kutumia uzoefu wao katika kuelimisha jamii  kupinga na kutokomeza vitendo vya ukatili kwa kundi hilo  katika jamii.

Akizungumza katika kikao cha kamati ya MTAKUWWA sehemu ya 2 kilichofanyika katika ukumbi wa siasa ni kilimo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Robert Masunya amesema anaamimi wadau na wajumbe kwa ngazi ya halmashauri watakwenda kuhakikisha wanakuwa sehemu ya kutokomeza ukatili.

Sauti ya Masunya

Awali Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bi Gladnss Amulike amesema muongozo wa MTAKUWWA II umezingatia ujumuishi wa ushiriki wa wanaume katika kupinga ukatili kuanzia  ngazi ya kaya.

Sauti ya Amulike

Kwa upande wake Loveness Mayingu ambaye ni Mkaguzi wa Jeshi la Polisi kitengo cha Dawati la jinsia na watoto amesema wao kama dawati wanaendelea kutoa elimu kwenye jamii ili kupumguza vitendo vya ukatili.

Sauti ya Mayingu

Ikumbukwe kuwa kikao hicho ni muendelezo wa  Mkoa wa Iringa  katika hatua na ngazi za Halmashauri zote  kutengeneza mpango mkakati wa  2024/25- 2028-29 ya kupambana na na  vitendo  fvya ukatili dhidi ya wanawake na watotokuanzia ngazi kata vijiji na mitaa.