Nuru FM

Mwongozo kuwainua kiuchumi wajane wazinduliwa

24 June 2025, 1:14 pm

Waziri Dorothy Gwajima akionesha Miongozo ya kuwasaidia wanawake wajane. Picha na Joyce Buganda.

Kutokana na changamoto wanazopitia wajane, serikali imeamua kufanya utafiti ili kuzitafutia ufumbuzi.

Na Adelphina Kutika

Serikali imezindua mwongozo mpya wa uratibu wa wajane wenye lengo la kulikomboa kundi hilo dhidi ya changamoto za ukatili wa kijinsia na vikwazo vya kiuchumi.

Mwongozo huo umetangazwa  na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wajane Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Iringa yenye kaulimbiu Isemayo “Tuimarishe Fursa za Kiuchumi Kuchochea Maendeleo ya Jamii.”

Sauti ya Gwajima

Kwa upande wake  mkuu wa Wilaya ya Kilolo Bi Rebecca Sanga Nsemwa  aliyemwakilisha mkuu wa mkoa wa Iringa amesema  maadhimisho hayo yamejumuisha  wajane kutoka  halmashauri zote tatu  yakiambatana na utoaji elimu ya fedha  na haki ya wajane

Sauti ya DC Rebecca

Nae mmoja wa wajane mkoani Iringa ameishauri jamii kuhakikisha waandika wosia ili kuondoa migogoro kwa familia  pindi wazazi wanapofariki.

Sauti ya Mjane

Hata hivyo mwongozo huo unalenga  kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii, kiuchumi na kisheria kwa wajane.