Nuru FM

Camfed kufanikisha elimu kwa mtoto wa kike

19 June 2025, 1:33 pm

Maafisa elimu na Viongozi wa Camfed wakiwa katika picha ya pamoja. picha na Chacha Robert

Mipango ya elimu kwa Mtoto wa kike imeanza Kutekelezwa Nchini Ili kukuza ustawi.

Na Joyce Buganda

Maafisa elimu  nchini wametakiwa kutekeleza miradi  ya Campagn For Female Educatiom CAMFED ili kufanikisha malengo ya mtoto wa kike kupata elimu bora kwa ustawi wa maisha na jamii kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo ya siku 2 yaliofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo Manispaa ya Iringa  mgeni rasmi  mkurugenzi wa idara ya usimamizi wa limu kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI  Suzan Nussu amesema maafisa hao wakasimamie vyema ipasavyo ardhi walizonazo kwa ajili ya miradi iliaonzishwa na shirika la CAMFED.

Sauti ya Suzan Nussu

Aidha Mkurugenzi wa Miradi na ushirikiano kutoka shirika lisilokuwa la kiserikali Campaign For Female education  CAMFED Anna Sawaki amesema mradi upo katika mikoa 10 na halmashauri 35 wamekutana kujadili juu ya utekelzaji wa miradi ya elimu ambayo inafanywa na CAMFED.

Sauti ya Anna Sawaki – Mkurugenzi

Kwa upande wao baadhi ya maafisa elimu wamesema  wanaendelea kushirikiana na  CAMFED ili kuemdeelea kuborha na kutimiza ndoto ya mtoto wa kike nchini.

Sauti ya Maafisa Elimu