Nuru FM

Kituo cha afya Mninga kuhudumia zaidi ya wananchi elfu 15

26 May 2025, 12:34 pm

Muonekano wa kituo Cha Afya Cha Mninga Wilaya ya Mufindi. Picha na Ayoub Sanga

Wananchi wanaotembea umbali mrefu kufuata huduma za afya wataanza kuneemeka na huduma za afya.

Na Ayoub Sanga

Zaidi ya shilingi milioni 400 zimetumika katika ujenzi wa Kituo cha afya cha Mninga kilichopo kata ya Mninga, Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.

Akiwasilisha taarifa mbele ya wajumbe wa Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa Afisa Mtendaji kata ya Mninga Bi Addah Lwangili amesema jumla ya fedha zilizopokelewa kwajili ya ujenzi  wa kituo cha Afya Mninga ni shilingi million 498.

Sauti ya Adda Afisa Mtendaji

Akiwa ameongozana na kamati ya siasa Mkoa wa Iringa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Peter Serukamba, ametoa wito kwa wakandarasi wanaojenga jengo la kisasa la mama na mtoto kuhakikisha linakamilika kabla ya mwezi wa 9 ili kuwarahisishia akina mama kupata huduma kwa wakati.

Sauti ya Serukamba RC Iringa

Akizungumza na wananchi waliokusanyika katika kituo hicho, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa Daud Yassin amesema kuwa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imejipanga kuboresha huduma za msingi, ikiwamo afya, ili kuwafikia wananchi wote kwa urahisi na ufanisi.

Sauti ya Daudi Yaasin Mwenyekiti CCM

Aidha Kituo hicho kinatarajiwa kuhudumia zaidi ya wananchi 15,000 waliokuwa wakikumbana na changamoto ya upatikanaji wa huduma za afya, ikiwemo kutembea zaidi ya kilomita 15 kufuata matibabu kama ambavyo hapa wananchi wakieleza

Sauti ya Wananchi Mninga

Hata hivyo Kituo cha afya cha Mninga kinajumuisha majengo ya wagonjwa wa nje (OPD), maabara, wodi ya wazazi, chumba cha upasuaji, na wodi za kulaza wagonjwa, hivyo kutarajiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo vya mama na mtoto na kuongeza ustawi wa jamii kwa ujumla.